Last Updated on 22/09/25 by Tabibu Fadhili Paulo
Dalili za bawasiri
Bawasiri dalili zake zinaweza kufanana kidogo na dalili za mtu anayeanza kuumwa vidonda vya tumbo. Nazo ni pamoja na zifuatazo :
1. Maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa
2. Kinyesi kunuka damu wakati wa kujisaidia
3. Muwasho sehemu ya tundu la haja kubwa
4. Uvimbe au kinyama kujitokeza sehemu ya tundu la haja kubwa
5. Haja kubwa yaweza kujitokea tu muda wowote
6. Kupungukiwa damu
7. Baada ya kupata haja kubwa unaweza usiishi tumbo kupungua
8. Maambukizi
Unapoona kuna damu inavuja mahala pa haja kubwa ama unapotoa haja, basi nashauri nenda haraka hospital kuonana na Daktari na kufanya vipimo, hasa kama tatizo ni limekutokea kwa mara ya kwanza.
Hata hivyo siyo kila kuvuja kwa damu kwenye sehemu ya haja kubwa inaweza kuwa ni bawasiri, wakati mwingine yaweza kuwa ni dalili za Saratani ya utumbo mpana .